TUMEHAMA / WE HAVE MOVED

TAFADHALI TEMBELEA TOVUTI YETU MPYA WWW.JAMIIPRODUCTION.COM (bofya hapa)

PLEASE VISIT OUR NEW WEBSITE WWW.JAMIIPRODUCTION.COM (click here)

TUMEHAMA. TAFADHALI TEMBELEA TOVUTI YETU MPYA WWW.JAMIIPRODUCTION.COM..........WE HAVE MOVED. PLEASE VISIT OUR NEW WEBSITE WWW.JAMIIPRODUCTION.COM

[AUDIO]: DAKIKA 90 ZA DUNIA. "Tiba" ya virusi vya UKIMWI kwa mtoto wa pili

Photo Credits: Fox 44
Mwezi wa tatu mwaka jana, madaktari nchini Marekani walitangaza kuwa mtoto mmoja kutoka jimbo la Missisipi nchini humo aliyezaliwa akiwa na virusi vya UKIMWI alitibiwa na kuonekana kutokuwa navyo tena.
Tangazo hilo lilizua mashaka makubwa kuwa yawezekana mtoto huyo hakuwa ameathirika na virusi hivyo licha ya kuwa Mama yake alikuwa mwathirika wa virusi.
Lakini madaktari waliendelea kusisitiza kuwa matibabu maalum waliyompa punde baada ya kuzaliwa yalimtibu.
Wiki hii, katika mkutano unaohusu masuala ya VIRUSI huko Boston, madaktari wametangaza kuwa mtoto wa pili aliyepata aina hiyo ya matibabu punde baada ya kuzaliwa amepimwa na kuonekana kutokuwa tena na virusi hivyo.

Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Hii ilikuwa ripoti ya Machi 8, 2014

[AUDIO]: Mjadala kuhusu Mitandao ya kijamii kutoka Jamii Production

Karibu katika kipindi hiki cha kwanza cha moja kwa moja (Live) kilichorushwa toka studio zetu za Washington DC
Katika kipindi hiki, mjadala ulikuwa juu ya MITANDAO YA KIJAMII.
Washiriki walikuwa Prof Nicholas Boaz. Mwalimu wa Mawasiliano kutoka Chuo kikuu cha Maryland.
Mzee
Emmanuel Muganda. Mtangazaji mkongwe aliyefanya kazi zaidi ya miaka 30
katika Idhaa za Sauti ya Amerika (VOA) na pia Denzel Musumba. Mmiliki wa
Border Media Group ambaye kwa miaka mingi amekuwa akitangaza kupitia
mitandao ya kiJamii
Kwa njia ya Skype tuliungana na Jeff Msangi. Mwandishi, Blogger na mwanaharakati aliyejiunga nasi kutoka Ontario Canada
Na kutoka nchini Tanzania tulimsikia mwakilishi wetu Ahmad James Nandonde aliyeongea na Mkuu wa Mkoa wa Mara na watu wengine.
Karibu sana

NB: Tunaomba radhi kwa ubora hafifu wa sauti katika baadhi ya sehemu za kipindi.

[AUDIO]: Kipindi cha FAMILIA...BAJETI KATIKA FAMILIA (Pt II)

Photo credits: moneymanagement.org

Karibu katika kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production.

Katika kipindi hiki, tumeingia katika sehemu ya pili ya mjadala kuhusu BAJETI KATIKA FAMILIA ambapo mbali na historia ya bajeti, pia tumesisitizwa kuhusu umuhimu wake, namna ya kulitekeleza na mengine mengi.

Wachangiaji studio walikuwa ni Amos Cherehani ambaye ni mtaalamu wa masuala ya fedha, Denzel Musumba na Mubelwa Bandio

KARIBU UUNGANE NASI

[AUDIO]: DAKIKA 90 ZA DUNIA: Kwanini Facebook imetumia dola bilioni 19 kununua WhatsApp?

Photo: Mobile88.com

Kama wewe ni mmoja wa wanaotumia njia ya mawasiliano iliyojipatia umaarufu ya
WhatsApp, basi ujue kuwa nawe ni miongoni mwa wateja takribani nusu
bilioni walioufanya mtandao huo kuwa maarufu zaidi duniani kwa kipindi
kifupi tu.
Ni umaarufu huu uliofanya kampuni kubwa ya mawasiliano
ya Facebook wiki hii kuona umuhimu wa kutumia dola za kimarekani bilioni
19 kununua WhatsApp.
Lakini kwanini kampuni itumie kiasi hicho kikubwa kwa kampuni kama hii?

Bahati Alex (L) na Mubelwa Bandio (R)

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Hii ilikuwa ripoti ya Februari 22, 2014

[AUDIO]: Kipindi cha familia kutoka Jamii Productuion...BAJETI KATIKA FAMILIA

Bwn Solomon, Sunday Shomari na Herriet Shangirai wakijadili jambo ndani ya studio za Jamii Production. Washington DC
Karibu katika kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production.
Katika kipindi hiki, tumejadili suala la BAJETI KATIKA FAMILIA.
umuhimu wake, namna ya kulitekeleza na mengine mengi.

Wachangiaji studio walikuwa ni Herriet Shangirai, Sunday Shomari, Solomon na Mubelwa Bandio
KARIBU UUNGANE NASI

Rekodi katika michuano ya Olimpiki Sochi

Michuano ya 22 ya Olimpiki ya majira ya baridi imeanza jana huko Sochi nchini Russia.
Mabadiliko mengi yametokea katika miaka sita na nusu ya maandalizi yake
Na wakati mamilioni ya watu duniani wakiwa wameelekeza macho na masikio yako huko, kujua nani atashinda nini na nani atavunja rekodi gani, tayari rekodi kubwa zaidi katika michuano hiyo imevunjwa hata kabla ya kuanza kwake.
Na tuipitie safari safari ya maandalizi ya michuano hii mpaka ilipofikia na baadhi ya vikwazo ilivyopambana navyo

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Februari 8, 2014