Dj Luke Joe alipofanya mahojiano na Jamii Production
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara alipokuwa akisisitiza jambo wakati wa mahojiano mafupi aliyofanya na Jamii Production kabla ya KUZINDUA RASMI shughuli za kutayarisha na kusambaza matangazo ya Radio na Video.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiwa na waanzilishi wa Jamii Production, Mubelwa Bandio (kulia) na Abou Shatry (kushoto)
Na......
Hakuna litajalokuwa na maana kama hatutajua namna ambavyo utendaji wetu unaathiri maisha yako kwa namna CHANYA na HASI
Wewe (msikilizaji, mtazamaji na msomaji wetu) ni mdau mkubwa wa kufanikisha hili.
Tuzidi kushirikiana
TWAWAPENDA
Msimamizi wa vipindi na mpigapicha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry akisisitiza jambo kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi
Mtayarishaji na Mtangazaji wa kipindi cha FAMILIA Georgina Lema akiwa "kitini"
Mmoja wa wawezeshaji wakuu wa Jamii Production Bwn Isidory Lyamuya wa Prestige Health Services akijaribu vitendea kazi vya kituo
Mhe. Waziri Mukangara akipokea maelezo ya utendaji wa kituo. Kushoto ni Afisa Ubalozi Mindi Kasiga
Mhe. Waziri akisikiliza RISALA ya Jamii Production
Mhe. Waziri Mukangara akijibu risala ya Jamii Production
Bwn Isidory Lyamuya akipata akipata picha ya pamoja na Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production
Bwn Isidory Lyamuya akipata mkono wa pongezi toka kwa Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production
Abou Shatry akipongezwa na Mhe Waziri Mukangara
"Mwanamama" Georgina Lema wa kipindi cha FAMILIA akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri
Mkurugenzi wa Mambo Jambo Radio Bwn Julius Makiri ambaye aliungana nasi katika uzinduzi huu rasmi akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri
Mhe. Waziri Dkt Fenella Mukangara na Afisa Habari katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Mindi Kasiga pamoja na wanaJAMII
Hakuna ZAWADI kubwa sawa na kilichofanyika. Na zawadi pekee tuliyonayo ni UPENDO. Ambao hauonyesheki wala haupimiki.
Lakini....tunapenda POPOTE UWAPO, UKUMBUKE SIKU YA LEO.
Na hivyo..twaomba KIKOMBE hiki kiwe kumbukumbu ya tukio hili kubwa kwetu
Abou Shatry akiwa mahala anapopatawala zaidi...
Kipindi cha FAMILIA kutoka kwa mtayarishaji Dada Ndeletwa C. Lema kinachorikodiwa kila Jumamosi katika Studio za Jamii Production, kutoka Washington DC, nchini Marekani
Mmoja wa wajangiaji wa kipindi cha Familia Mama Martha akichangia na kusikiliza maada inayohusu jitihada za malezi ya watoto ndani ya familia zetu, kilichotayarisha na Dada Ndeletwa C. Lema ndani ya Studio ya Jamii Production.
Mwanachangamoto yetu, fundi mitambo piamchangiaji wa kipindi maalum cha Familia k Mubelwa Bandio akichangia Jambo ndani ya Studio ya Jamii Production.
Mmoja wa wajangiaji wa kipindi cha Familia Dada Oliver Lyimo, akichangia na kusikiliza maada inayohusu jitihada za malezi ya watoto ndani ya familia zetu, kilichotayarisha na Dada Ndeletwa C. Lema ndani ya Studio ya Jamii Production.
Muongozaji wa kipindi cha Familia Dada Ndeletwa C. Lema akifafanua jambo
Mwanachangamoto yetu, fundi mitambo na pia muendeshaji kipindi maalum kuhusu tukio la ugaidi nchini Kenya Mubelwa Bandio akiwa mitamboni.
Wanaharakati wa Jumuiya ya waKenya DMV Mwalimu Mkawasi Mcharo Hall alipokua akufanya mahojiano na Jamii Production kuhusu shambulio la mauwaji ya Westgate Mall siku ya Jumamosi Sept 29 ndani ya Westgate Mall jijini Nairobi Kenya.
Moja kati ya wanaharakati wa Jumuiya ya waKenya DMV na pia Mtangazaji wa Redio ya theonemic Show Washington DC Ali Badawy akiwa makini katika kipindi ndani ya Studio ya Jamii Production iliopo Washaington DC nchini Marekani
Mwalimu Mkawasi Mcharo Hall akiwa makini katika kipindi ndani ya Studio ya Jamii Production iliopo Washaington DC nchini Marekani.
Mzee wa swahilivivilla Camera Man Abou Shatry akiwa na kilevi chake
Mzee wa Changamoto yetu nae pia akiwa katika kilevi chake
No comments:
Post a Comment